Habari zilizotufikia zinasema askari polisi watatu wameuwawa katika uvamizi wa majambazi katika Benki ya CRDB tawi la Mbande jijini Dar es salam mnamo saa moja na nusu jioni ya leo Jumanne Agosti 23, 2016.
Askari waliouwawa inasemekana ni E5761 CPL YAHAYA, F4660 CPL HATIBU NA G9544 PC TTITO.
Habari zinasema majambazi hayo yamepora SMG moja kabla ya kutokomea, na kwamba tukio hili limetokea wakati askari wakibadilishana lindo.
Mmoja wa askari waliouwawa alikuwa anaingia, mmoja alikuwa anatoka na mwingine alikuwa dereva. Inasemekana Majambazi hayo ambayo idadi yao haijajulikana hayakuingia ndani ya bank.
Paparazi blog ONEKANA MJANJA: SHARE HABARI HII KWA MARAFIKI ZAKO NA KATIKA MAGROUP YA WHATSAPP FREE (only for mobile)