Matonya ni mwanaume anayejua kuhonga, kwa mujibu wa mpenzi wake, Gigy Money.
Akizungumza katika kipindi cha Kubamba cha Times Fm Jumapili, Gigy aliweka wazi mahusiano yake na Matonya ambapo alimpigia simu ‘live’ redioni na kuzungumza kimahaba huku akijinasibu kwa dhati kuwa Matonya ni miongoni mwa wapenzi wake wanaohonga vizuri.
“Nimechoka kuulizwa kila siku juu ya Matonya ngoja nimpigie umsikie mwenyewe(anampigia)” alisema Gigy na kumpigia simu Matonya.
“Unajua nampenda sana Tonya kwa sababu anajua kuhonga aisee, namuelewa sana yani,” alimaliza.
Paparazi blog ONEKANA MJANJA: SHARE HABARI HII KWA MARAFIKI ZAKO NA KATIKA MAGROUP YA WHATSAPP FREE (only for mobile)