May 24, 2016

Nuh Mziwanda: Miaka mitatu ya kuwa na Shilole imenipoteza mambo mengi

13258956_1620055491649122_1622452524_n

Nuh Mziwanda amedai katika miaka mitatu aliyokuwa na uhusiano na Shilole amepoteza mambo mengi.
Akizungumzia issue hiyo Nuh amesema hakuna zaidi anachokumbuka kwenye uhusiano huo zaidi ya majuto.
“Kuna vitu muhimu sana ambavyo nimegundua ningeweza kuvifanya na ningekuwa nipo mbali sana,” amesema Nuh. Muimbaji huyo amesema uhusiano huo ulimfanya auchukulie poa muziki na hivyo kushindwa kutengeneza hit song.
Anasema Shilole alihakikisha katika muda wote waliokuwa nao Nuh asihit kwa uoga kuwa akiwa staa atamuacha.
“Yule [Shilole] alikuwa na trick nyingi za kunifanya mimi nijionee staa tayari, nijione mimi napendwa na watu au mimi muziki wangu unavuma kumbe bado halafu yeye huku muziki wake unaenda,” amesisitiza.
credit:bongo5

Paparazi blog
ONEKANA MJANJA: SHARE HABARI HII KWA MARAFIKI ZAKO NA KATIKA MAGROUP YA WHATSAPP FREE (only for mobile)

TUPE MAONI YAKO HAPA!